Hamia kwenye habari

Ni Nani Ambao Majina yao Yameandikwa Katika “Kitabu cha Uzima”?

Ni Nani Ambao Majina yao Yameandikwa Katika “Kitabu cha Uzima”?

Jibu la Biblia

 “Kitabu cha uzima,” pia huitwa “kitabu cha kukunjwa cha uzima” au “kitabu cha kumbukumbu,” kina majina ya watu ambao watapata zawadi ya uzima wa milele. (Ufunuo 3:5; 20:12; Malaki 3:16) Mungu anaamua majina hayo kwa kutegemea imani na ushikamanifu wao kwake.​—Yohana 3:16; 1 Yohana 5:3.

 Mungu amewaweka katika kumbukumbu watumishi wake waaminifu, kana kwamba anaandika majina yao kwenye kitabu, “tangu kuwekwa kwa msingi wa ulimwengu” wa wanadamu. (Ufunuo 17:8) Inaonekana kwamba jina la mwanamume mwaminifu Abeli, lilikuwa la kwanza kuandikwa katika kitabu hicho cha uzima. (Waebrania 11:4) Kitabu hicho si orodha tu ya majina, badala yake kinaonyesha kwamba Yehova ni Mungu mwenye upendo ambaye “anawajua walio wake.”—2 Timotheo 2:19; 1 Yohana 4:8.

Je, majina yanaweza kufutwa kutoka katika “kitabu cha uzima”?

 Ndiyo. Mungu alisema hivi kuhusu Israeli la kale “Yeyote ambaye amenitendea dhambi, nitamfutilia mbali kutoka katika kitabu changu.” (Kutoka 32:33) Lakini ikiwa tutaendelea kuwa waaminifu, majina yetu yatabaki kwenye “kitabu cha kukunjwa cha uzima.”​—Ufunuo 20:12.