AMKENI! Na. 3 2017 | Je, Kweli Biblia Ni Kitabu cha Mungu?
Je, Biblia ni kitabu cha Mungu? Au ni kitabu kilichojaa mawazo ya wanadamu?
Toleo hili la “Amkeni!” linazungumzia mambo matatu yanayothibitisha kwamba Biblia ni kitabu cha Mungu.
HABARI KUU
Biblia—Je, Kweli ‘Imeongozwa na Roho ya Mungu’?
Baadhi ya watu wanafikiri kwamba kwa njia fulani Biblia ina uhusiano na Mungu. Wengine wanaiona kuwa mkusanyo wa hekaya za kale, historia, na mafundisho ya wanadamu.
HABARI KUU
Biblia—Ni Sahihi Katika Nyanja Zote
Biblia ilielezea kwa usahihi habari kuhusu dunia muda mrefu kabla ya wanasayansi kugundua mambo hayo. Zaidi ya hilo, ilitabiri kuhusu kuinuka na kuanguka kwa falme mbalimbali, na pia inatoa majibu yenye kuridhisha ya maswali muhimu maishani.
KUTOKA KWA WASOMAJI WETU
Umuhimu wa Kazi za Nyumbani
Je, unasita kuwapatia watoto wako kazi za nyumbani? Ikiwa ndivyo, ona jinsi ambavyo kazi hizo zinaweza kuwafundisha uwajibikaji na kuwaletea furaha.
Mfumo wa Neva Ulio Tumboni—Je, Ni “Ubongo wa Pili” Katika Mwili Wako?
Sehemu kubwa ya “karakana hii tata ya kemikali” inapatikana tumboni. Inafanya kazi gani hasa?
MAHOJIANO
Mtaalamu wa Programu za Kompyuta Anaeleza Kwa Nini Anamwamini Mungu
Alipoanza kazi yake akiwa mtaalamu wa hesabu, Dakt. Fan Yu aliamini mageuzi. Sasa anaamini kwamba uhai ulibuniwa na kuumbwa na Mungu. Kwa nini?
MAONI YA BIBLIA
Malaika
Malaika wamezungumziwa katika vitabu mbalimbali, michoro, na sinema. Maandiko yanasema nini kuwahusu?
JE, NI KAZI YA UBUNI?
Manyoya ya Fisi Maji wa Baharini
Baadhi ya wanyama wanaoishi majini wana tabaka la mafuta linalowasaidia kudumisha joto. Fisi maji wa baharini hutumia mbinu nyingine.
Habari Zaidi Mtandaoni
Nifanye Nini Ili Nipate Uhuru Zaidi?
Wewe unafikiri kwamba uko tayari kutendewa kama mtu mzima, lakini wazazi wako hawaoni hivyo. Unaweza kuchukua hatua gani ili wakuamini zaidi?
Ni Nani Aliyeitunga Biblia?
Ikiwa Biblia iliandikwa na wanadamu, je ni sahihi kuiita Neno la Mungu? Biblia ina mawazo ya nani?