Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Njia ya 5—Jitie Moyo na Uwachochee Watu wa Familia

Njia ya 5—Jitie Moyo na Uwachochee Watu wa Familia

Njia ya 5—Jitie Moyo na Uwachochee Watu wa Familia

“Mtu aliye mwerevu atatenda kwa ujuzi.” (Methali 13:16) Kupata habari za msingi kuhusu afya kunaweza kukuchochea ufanye mabadiliko yanayohitajiwa ili wewe na familia yako muwe na afya bora.

◯ Endelea kujifunza. Katika nchi nyingi, shule za umma na za kibinafsi huwa na programu na vitabu vinavyozungumzia habari mbalimbali kuhusu afya. Tumia maandalizi hayo, na ujifunze jinsi ya kuboresha afya yako na kuepuka kuihatarisha. Uwe na akili iliyofunguka, na uwe tayari kufanya marekebisho machache.

Mazoea mazuri unayojifunza na kufuata yatawanufaisha watoto wako na watoto wao pia. Wazazi wanapoweka mfano mzuri kuhusu kula vyakula vyenye lishe, usafi, mazoea mazuri ya kulala, kufanya mazoezi, na kuzuia magonjwa, watoto wao watanufaika.—Methali 22:6.

◯ Ni nini zaidi linalohitajiwa? Kutaka tu kuwa na afya nzuri hakutoshi. Inaweza kuwa vigumu kuacha mazoea mabaya ya muda mrefu, na mara nyingi unahitaji kujitahidi sana kufanya hata mabadiliko madogo. Hata wanapokabili hatari ya kupatwa na ugonjwa mbaya au kifo, huenda watu fulani wasifanye mambo ambayo wanajua yatawafaidi. Ni nini kinachoweza kuwachochea kuchukua hatua? Sisi sote tunahitaji kuzingatia kusudi kuu la maisha.

Wenzi wa ndoa wanahitaji kuwa na afya nzuri na wenye nguvu ili waendelee kusaidiana. Wazazi wanataka kuendelea kuwategemeza na kuwazoeza watoto wao. Watoto wenye umri mkubwa wanahitaji kuwatunza watu wa ukoo waliozeeka. Na kuongezea hayo, tunataka kuinufaisha jamii badala ya kuwa mzigo. Mambo hayo yote yanahusisha kuwapenda na kuwajali wengine.

Kichochezi kikubwa ni kuthamini na kujitoa kwa Muumba wetu. Wale wanaomwamini Mungu wanataka kulinda zawadi yake ya uhai ambayo ni yenye thamani sana. (Zaburi 36:9) Tunapokuwa na afya, tunaweza kumtumikia Mungu kwa nguvu. Hiyo ndiyo sababu kubwa zaidi inayotuchochea tutunze afya yetu.

[Blabu katika ukurasa wa 8]

Furahia faida za kuwa na afya nzuri