Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

‘Hekima Inapaaza Sauti’​—Je, Unaisikia?

‘Hekima Inapaaza Sauti’​—Je, Unaisikia?

“Je, hekima haendelei kupaaza sauti, na utambuzi haendelei kutoa sauti yake? Husimama juu ya vilele, kando ya njia, kwenye makutano ya barabara. . . . Kwenye kiingilio cha malango huendelea kulia kwa sauti kubwa.” METHALI 8:1-3.

HEKIMA ni sifa muhimu sana. Bila hekima tunaweza kufanya makosa mengi ya kipumbavu. Lakini tunaweza kupata wapi hekima ya kweli? Mwandikaji wa kitabu cha Methali alizungumzia kuhusu hekima isiyo na kifani ya Muumba wetu. Isitoshe, karibu wanadamu wote wanaweza kupata hekima hiyo katika kitabu fulani cha pekee sana, Biblia. Fikiria mambo yafuatayo:

  • Kulingana na kitabu kinachoitwa The World Book Encyclopedia, Biblia ndicho “kitabu kilichosambazwa zaidi katika historia.” “Imetafsiriwa mara nyingi zaidi, na katika lugha nyingi kuliko kitabu kingine chochote.” Sasa Biblia inapatikana ikiwa nzima au kwa sehemu katika lugha karibu 2,600, kwa hiyo zaidi ya asilimia 90 ya watu ulimwenguni wanaweza kuipata.

  • Vilevile hekima “huendelea kulia kwa sauti kubwa” kwa njia halisi zaidi. Andiko la Mathayo 24:14 linasema hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho [wa ulimwengu huu] utakapokuja.”

Hiyo “habari njema” ni hekima ya kweli kwa sababu inakazia jinsi Mungu atakavyotatua matatizo ya wanadamu kwa hekima kupitia Ufalme Wake. Ufalme huo ni serikali ya Mungu ambayo itaitawala dunia yote, naam, ulimwengu mmoja, serikali moja. (Danieli 2:44; 7:13, 14) Ndiyo sababu Yesu Kristo alisali hivi: “Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.”—Mathayo 6:9, 10.

Mashahidi wa Yehova wanafurahi sana kutangaza Ufalme wa Mungu katika nchi 239! Kwa kweli, hekima—hekima ya Mungu—‘inalia kwa sauti,’ hata “kwenye kiingilio cha malango.” Je, unaisikia?