Kuhusu Ufalme wa Mungu
Tunayojifunza Kutoka Kwa Yesu
Kuhusu Ufalme wa Mungu
Ufalme wa Mungu ni nini?
Ufalme wa Mungu ni serikali ambayo itatawala dunia yote. Yesu alisema: “Basi, ninyi msali hivi: . . . ‘Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.’”—Mathayo 6:9, 10; Danieli 2:44.
Ni nani watakaokuwa watawala wa Ufalme wa Mungu?
Yesu alizaliwa ili awe Mtawala wa Ufalme wa Mungu. Malaika alimwambia hivi mama ya Yesu: “Yehova Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake.” (Luka 1:30-33) Kwa kuongezea, Yesu alichagua baadhi ya wafuasi wake ili watawale pamoja naye. Aliwaambia mitume wake: “Ninyi ndio mmeshikamana nami katika majaribu yangu; nami ninafanya agano pamoja nanyi, sawa na vile Baba yangu alivyofanya agano pamoja nami, kwa ajili ya ufalme.” (Luka 22:28, 29; Danieli 7:27) Jumla ya wafuasi 144,000 wa Yesu ndio watakaotawala pamoja naye.—Ufunuo 5:9, 10; 14:1.
Serikali hiyo itakuwa wapi?
Ufalme wa Mungu utatawala kutoka mbinguni. Yesu aliwaambia hivi wanafunzi wake: “Nikienda na kuwatayarishia ninyi mahali [mbinguni], nitakuja tena nami nitawapokea ninyi nyumbani kwangu mwenyewe, ili mahali nilipo mimi, ninyi pia muwe hapo. . . . Ninaenda kwa Baba.”—Yohana 14:2, 3, 12; Danieli 7:13, 14.
Ufalme wa Mungu utachukua hatua gani ili kukomesha uovu?
Yesu atawaondoa watu wote waovu duniani. Yesu alisema hivi: “Wakati Mwana wa binadamu [Yesu] atakapofika katika utukufu wake, na malaika wote Mathayo 25:31-34, 46.
pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mmoja kutoka kwa mwenzake . . . Na hawa [waovu] watakatiliwa mbali milele, lakini waadilifu wataingia katika uzima wa milele.”—Ni nani watakaoishi duniani wakiwa raia wa Ufalme huo?
Yesu alisema: “Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watairithi dunia.” (Mathayo 5:5; Zaburi 37:29; 72:8) Dunia itajaa watu ambao hata sasa wanajifunza kupendana. Yesu aliwaambia hivi wafuasi wake: “Ninawapa ninyi amri mpya, kwamba mpendane; kama vile ambavyo nimewapenda ninyi, ninyi nanyi mpendane vivyo hivyo. Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.”—Yohana 13:34, 35.
Ufalme wa Mungu utawafanyia nini wanadamu duniani?
Yesu ataponya magonjwa yanayowakumba wanadamu. Yesu alipokuwa duniani, alizungumza na umati wa watu kuhusu “ufalme wa Mungu, naye akawaponya wale wanaohitaji kuponywa.” (Luka 9:11) Baada ya kumuona Yesu aliyefufuliwa katika maono, mtume Yohana alisema: “Nikaona mbingu mpya na dunia mpya . . . Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha ufalme ikisema: ‘Tazama! Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu . . . Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena.’”—Ufunuo 21:1-4.
Ufalme wa Mungu utaifanya dunia iwe Paradiso. Mtenda-maovu mmoja aliyeuawa pamoja na Yesu alisema: “Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.” Naye Yesu akamwambia: “Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”—Luka 23:42, 43; Isaya 11:4-9.
Kwa habari zaidi, ona sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? *
[Maelezo ya Chini]
^ fu. 16 Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.