Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Mungu Ana Jina?

Je, Mungu Ana Jina?

Je, Mungu Ana Jina?

Watu wengi wanajibu hivi:

▪ “Jina lake ni Mungu tu.”

▪ “Hana jina lake mwenyewe.”

Yesu alisema nini?

▪ “Basi, ninyi msali hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.’” (Mathayo 6:9) Yesu aliamini kwamba Mungu ana jina.

▪ “Nimewajulisha jina lako nami nitalijulisha, ili upendo ulionipenda nao upate kuwa ndani yao nami katika muungano pamoja nao.” (Yohana 17:26) Yesu aliwajulisha watu jina la Mungu.

▪ “Hamtaniona kamwe mpaka mtakaposema, ‘Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!’” (Luka 13:35; Zaburi 118:26) Yesu alitumia jina la Mungu.

MUNGU mwenyewe anatuambia jina lake. Imeandikwa kuwa alisema hivi: “Mimi ni Yehova.” * (Kutoka 6:2, Union Version) Katika Kiswahili jina Yehova ndilo linalojulikana zaidi kuwa limetafsiriwa kutokana na jina la Kiebrania ambalo Mungu alijipa. Huenda ukashangaa kujua kwamba jina hilo la pekee la Kiebrania linapatikana mara elfu kadhaa katika hati za kale za Biblia. Kwa kweli, linapatikana mara nyingi zaidi kuliko jina lingine lolote linalotajwa katika Biblia.

Watu fulani wanaweza kujibu swali, “Mungu anaitwa nani?” kwa kusema, “ni Mungu tu.” Kwa kweli, jibu hilo halitoi habari kamili. Ni kama unapoulizwa, “Ni nani aliyeshinda uchaguzi?” ujibu, “ni mgombeaji.” Majibu hayo hayatoi habari kamili, kwa kuwa “Mungu” na “mgombeaji” si majina ya watu.

Kwa nini Mungu alituambia jina lake? Alifanya hivyo ili tumjue vizuri zaidi. Kwa mfano, mtu anaweza kuitwa Daktari, Baba, au Babu ikitegemea ni nani anayemwita. Majina hayo ya cheo yanafunua jambo fulani kumhusu. Lakini jina la mtu huyo linatukumbusha mambo yote tunayojua kumhusu. Vivyo hivyo, majina ya cheo kama vile Bwana, Mweza-Yote, Baba, na Muumba yanatukumbusha mambo tofauti-tofauti kuhusu utendaji wa Mungu. Lakini ni jina lake tu, Yehova, linalotukumbusha mambo yote tunayojua kumhusu. Kwa kweli, ili kumjua Mungu lazima ujue jina lake.

Si muhimu tu kujua jina hilo bali ni muhimu pia kulitumia. Kwa nini? Kwa kuwa Biblia inatuambia: “Kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.”—Waroma 10:13; Yoeli 2:32.

[Maelezo ya chini]

^ fu. 9 Kwa maelezo kuhusu maana ya jina la Mungu, na pia kwa nini tafsiri fulani za Biblia hazitumii jina hilo, unaweza kusoma ukurasa wa 195-197 katika kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Mtu anaweza kuitwa Daktari, Baba, au Babu ikitegemea ni nani anayemwita. Lakini jina la mtu huyo linatukumbusha mambo yote tunayojua kumhusu