Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Namna ya Kuzungumuza na Kijana Wako Kuhusu Tabia ya Kutuma Mambo ya Ngono Kupitia Simu

Namna ya Kuzungumuza na Kijana Wako Kuhusu Tabia ya Kutuma Mambo ya Ngono Kupitia Simu

TATIZO

Umesikia kwamba tabia ya kutuma mambo ya ngono kupitia simu ao telefone imeenea sana kati ya vijana. Unaweza kujiuliza, ‘Kijana wangu anafanya hivyo?’

Unataka kuzungumuzia jambo hilo na kijana wako​—lakini utafanya hivyo namna gani? Mbele ya kujibia, chunguza sababu gani vijana fulani wamejiingiza katika tabia hiyo ya kutuma mambo ya ngono kupitia simu na sababu gani unaweza kuhusika katika jambo hilo. *

SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?

  • Vijana fulani wanatuma ujumbe wenye kuamusha tamaa ya ngono ili kumuchezea kimapenzi mutu fulani ambaye wanamupenda.

  • Katika hali fulali, kijana mwanamuke anatuma picha yake mwenyewe inayoamusha hamu ya ngono kwa sababu anakazwa na kijana mwanaume kufanya hivyo.

  • Wakati fulani kijana mwanaume anaweza kutuma picha ya kijana mwanamuke inayoamusha hamu ya ngono ili kuwafurahisha marafiki wake ao kulipiza kisasi kisha urafiki wake kuvunjika pamoja na kijana huyo mwanamuke.

Hata sababu iwe gani, kijana aliye na simu anaweza kuingia katika shida nyingi. Kitabu fulani kinasema kwamba “kwa kutuma tu habari ao picha, maisha yanabadilika milele.” (CyberSafe)

Watu wengi hawatambue kwamba mara tu picha inapotumwa, mutu ambaye aliituma hana tena uwezo wa kujua namna picha hiyo itatumiwa. Katika hali moja, kulingana na habari fulani iliyotolewa na Shirika la Upelelezi la Amerika (FBI), kijana mwanamuke wa miaka 18 “alimutumia rafiki yake mwanaume picha yake akiwa uchi. Rafiki yake huyo mwanaume aliitumia pia kwa mamia ya vijana kwenye masomo. Inawezekana wanafunzi wengine, ambao waliona picha hiyo walimushambulia kijana huyo mwanamuke, na kisha akajiua.”

Kutuma mambo ya ngono kupitia simu kunaweza kutokeza pia mambo ya kisheria. Kwa mufano, mahali fulani, watoto ambao hawajakuwa watu wazima ambao waliwatumia watoto wenzao picha zinazoamusha tamaa ya ngono wameshitakiwa kuwa na kosa la kufanya ponografia ya watoto na waliombwa wajiandikishe kuwa wenye makosa ya kingono. Wewe muzazi, unaweza pia kuhusika ikiwa jina lako linapatikana kwenye oroza ya majina ya watu yaliyo katika simu ya mutoto wako ao ikiwa hauchukue hatua fulani ili kumuzuia mutoto wako kutuma mambo ya ngono kupitia simu.

MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Uweke sheria zilizo wazi. Hata ikiwa hauwezi kuchunguza kabisa namna kijana wako anavyotumia simu yake, unaweza kuhakikisha kwamba anajua sheria na pia matokeo mabaya ya kuvunja sheria hizo. Kumbuka pia kwamba wewe ukiwa muzazi, una haki ya kuchunguza namna kijana wako anavyotumia simu yake.​—Kanuni ya Biblia: Waefeso 6:1.

Umusaidie kijana wako afikirie tatizo la kutuma mambo ya ngono kupitia simu. Unaweza kusema: “Watu wana maoni tofauti-tofauti kuhusu kutuma mambo ya ngono kupitia simu. Wewe una maoni gani kuhusu jambo hilo?” “Ni picha za aina gani ambazo unafikiri hazifae?” “Mahali fulani inaonekana kuwa ni kuvunja sheria ikiwa kijana mudogo anatuma picha ya kijana mwengine mudogo aliye uchi. Wewe unawaza kuna ubaya kufanya hivyo?” “Sababu gani ni vibaya kutuma mambo ya ngono kupitia simu?” Sikiliza kwa uangalifu maoni ya kijana wako, na umusaidie afikirie matokeo mabaya ya kutuma mambo ya ngono kupitia simu.​—Kanuni ya Biblia: Waebrania 5:14.

Umusaidie kijana wako afikirie matokeo mabaya ya kutuma mambo ya ngono kupitia simu

Utoe mifano ya hali zinazoweza kutokea. Unaweza kumuelezea binti yako hivi: “Tuseme kwa mufano kijana mwanaume anamukaza kijana mwanamuke ‘amutumie mambo ya ngono kupitia simu.’ Kijana huyo mwanamuke anaweza kufanya nini? Atakubali tu ili urafiki wao usivunjike? Je, atakataa kumutumia mambo ya ngono lakini akubali kuchezeana naye kimapenzi? Atakatiza urafiki huo? Ataambia mutu muzima jambo hilo?” Saidia binti yako afikiri juu ya hali hiyo. Bila shaka, unaweza kutumia njia kama hiyo ili kufikiri na kijana wako mwanaume.​—Kanuni ya Biblia: Wagalatia 6:7.

Umusaidie kijana wako aelewe faida ya kuwa na sifa ao tabia nzuri. Umuulize maulizo kama haya: Je, kuwa na sifa nzuri ni jambo la maana kwako? Ungependa kujulikana kwa sifa gani? Unaweza kujisikia namna gani ikiwa unamuvunjia heshima mutu fulani kwa kutumia watu wengine picha isiyofaa ya mutu huyo? Unaweza kujisikia namna gani ikiwa unashikamana na mambo yaliyo sawa? Umusaidie kijana wako ‘awe na zamiri njema.’​—1 Petro 3:16.

Umuonyeshe kijana wako mufano muzuri. Biblia inasema kwamba hekima inayotoka kwa Mungu ni safi kiadili na haina unafiki. (Yakobo 3:17) Je, tabia zako zinaonyesha kwamba unaishi kulingana na maneno hayo? Kitabu kimoja kinasema hivi: “Tunahitaji kuonyesha mufano muzuri sisi wenyewe kwa kuacha kutazama picha na kufungua vituo vya Internete ambavyo vinaweza kuonwa kuwa visivyofaa na vilivyo kinyume cha sheria. (CyberSafe)

^ “Kutuma mambo ya ngono” kunatia ndani kutuma ujumbe, picha, ao video za ngono kupitia simu. Ili kupata habari zaidi juu ya jambo hilo, fungua adresi yetu ya Internete jw.org na usome habari “Vijana Wanauliza​—Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kutuma Mambo ya Ngono Kupitia Simu?”​—Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > VIJANA.