Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Ulimwengu

Habari Fulani za Ulimwengu

Ulimwengu

“Kila mwaka, watoto wadogo karibu milioni 3 wanakufa katika mwezi wa kwanza wa maisha yao, wengi wao wanakufa ijapokuwa kulikuwa uwezekano wa kuepuka kifo. Zaidi ya watoto milioni moja kati yao wanakufa siku ambayo walizaliwa.”​—⁠Save the Children International.

Uingereza

Shirika la Afya la Uingereza linaonyesha kwamba katika mwaka wa 2011, kulikuwa ongezeko la vifo vya watu kwa sababu ya kuchafuliwa kwa hewa katika maeneo 15 yaliyo ndani ya muji wa Londres. Jambo la kushangaza ni kwamba watu wanasema motokari zinazotumia mafuta ya diesel hazichafue hewa kwa sababu zinatumia mafuta kidogo na zinatoa dioksidi ya kaboni ndogo sana. Hata hivyo, vitu 91 juu ya 100 vinavyochafua hewa katika eneo hilo vinatokana na motokari zinazotumia mafuta ya diesel.

Urusi

Kulingana na uchunguzi uliofanywa na Shirika Linaloshugulikia Maoni ya Watu la Urusi katika mwaka wa 2013, Warusi karibu 52 juu ya 100 waliojiita kuwa Wakristo wa dini ya Ortodoksi walisema kwamba hawajasoma hata kidogo sehemu moja ya Biblia, na 28 juu ya 100 walisema kwamba wanasali mara chache sana.

Afrika

Ripoti moja ya Benki Kubwa ya Dunia inaonyesha kwamba kugombania mashamba kunazuia watu kukomalisha chakula na kunaongeza umaskini. Nusu ya udongo wa dunia usiolimwa, ni kusema, hektari milioni 202, unapatikana katika Afrika, kontinenti inayosemekana kuwa na uwezo wa kutoa chakula kingi, lakini ambayo inatoa tu sehemu 25 juu ya 100.

Amerika

Masomo mengi ya musingi, ya segondari, na ya juu yanatumia sasa vyombo vya kielektroniki kuliko kutumia vitabu. Vyombo hivyo vina habari nyingi za kusoma, programu za ordinatere, na mambo mengine. Lakini, ijapokuwa njia hiyo haina garama nyingi ya feza, watu wana mashaka nayo.