Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mu muji wa Ninawi mulikuwa majengo na minara mikubwa

Ulijua?

Ulijua?

Ni nini ilipata muji wa Ninawi kisha siku za Yona?

KARIBU na mwaka wa 607 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Ashuru ilifikia kuwa Ufalme mukubwa zaidi mu dunia yote. Kulingana na mafasirio yenye kuwa ku site ya Enternete ya Nyumba ya Vitu vya Kukumbuka ya Uingereza, “Ashuru ilianzia upande wa mangaribi wa Kipro, mupaka upande wa mashariki wa Iran, na wakati fulani ilitia ndani Misri.” Ninawi muji wake mukubwa, njo ilikuwa muji mukubwa zaidi mu dunia yote. Ninawi ilikuwa na minara mikubwa, bustani za muzuri, nafasi na maktaba mingi kubwakubwa. Maandishi ya ku ukuta ya mu Ninawi ya zamani, inaonyesha kama Mufalme Ashurbanipal alijiita “Mufalme wa dunia,” sawa vile tu wafalme wengine wa Ashuru. Ile wakati, ilionekana sawa vile haiwezekane kuangusha Ashuru na Ninawi.

Serikali kubwa ya ulimwengu ya Ashuru njo ilikuwa Ufalme mukubwa zaidi mu dunia yote ile wakati

Lakini, wakati mamlaka ya Ashuru ilifikia kuwa kubwa zaidi, Yehova alitabiri hivi kupitia nabii wake Sefania: ‘[Yehova] ataharibu . . . Ashuru, na atafanya Ninawi ikuwe ukiwa, kama eneo lenye kukauka la jangwa.’ Pia, Nahumu nabii mwingine wa Yehova alitabiri hivi: “Munyanganye feza, munyanganye zahabu! . . . Muji hauna kitu ndani yake, umeachwa ukiwa, umeharibiwa! . . . Kila mutu mwenye atakuona atakukimbia na kusema, ‘Muji wa Ninawi umeharibiwa!’” (Sef. 2:13; Nah. 2:9, 10; 3:7) Kisha kusikia ile maneno ya unabii, pengine watu walijiuliza hivi: ‘Ile itawezekana kabisa? Ashuru iko na nguvu sana, itawezekana kweli kuiangusha?’ Ilionekana kama ile haiwezekane.

Ninawi ilifikia kuachwa ukiwa!

Hata vile, Ashuru iliangushwa! Karibu na mwisho wa mwaka wa 600 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Wababiloni na Wamedi waliangusha Ashuru. Ku mwisho, watu hawakuishi tena mu Ninawi na walifikia kuisahau! Kitabu moja ya Metropolitan Museum of Art mu New York, inasema kama, “Ninawi ilifikia kuzikwa, na watu walijua habari ya Ninawi, kupitia tu Biblia.” Kulingana na The Biblical Archaeology Society, ku mwanzo wa miaka ya 1800, “hakuna hata mutu mwenye alijuaka kama Ninawi, muji mukubwa wa Ashuru, ulikuaka.” Lakini kisha pale, mu 1845, Muakiolojia Austen Henry Layard alianza kuchimba mabomoko ya Ninawi. Mabomoko yenye ilivumbuliwa mu ile eneo, ilihakikisha kama Ninawi ilikuwa muji ya muzuri sana.

Kuona vile maunabii kuhusu muji wa Ninawi ilitimia, kunatupatia uhakika kama maunabii ingine ya mu Biblia yenye inahusu kuharibiwa kwa serikali zote za ulimwengu itatimia pia.​—Da. 2:44; Ufu. 19:15, 19-21.