Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Sababu gani wakati wa zamani watu walitumia lami (gudro) kama saruji ao sima katika ujenzi?

Biblia inasema kama wajenzi wa munara wa Babeli walitumia ‘matofali kuwa mawe yao, lakini lami ikawa saruji yao.’​—Mwanzo 11:3.

Lami haitengenezwe, inatoka katika petroli ndani ya udongo, na inapatikana kwa uwingi katika Mesopotamia, ambapo inatoka katika udongo na kisha inajiganda. Uwezo wake wa kunata ulijulikana tangu wakati wa zamani. Kitabu kimoja kinasema kama lami ilikuwa “yenye kufaa ili kujenga nyumba za matofali yenye kuchomwa.”

Habari moja katika gazeti Archaeology inaeleza matembezi fulani ya hivi karibuni yaliyofanywa kwenye mabomoko ya munara unaoitwa ziggourat katika muji wa zamani wa Uru, huko Mesopotamia. Muandikaji wa gazeti hilo anasema kama “lami iliyotumiwa kama saruji, iliyotumiwa kwa mara ya kwanza katika eneo kubwa linalotoa Petroli kusini mwa Irak, ingali inaonekana kati ya matofali yenye kuchomwa.” “Lami iliyo kama mafuta ya petroli, ambayo ni nyeusi na yenye kunata, iliwafanya watu zamani katika eneo hilo wawe wenye kusikilizana, lakini leo, inakuwa sababu ya vita na mivurugo. Kutumia lami kama saruji na kama lipu kulisaidia sana ili matofali ya udongo wa eneo la Sumeria ambayo yalikuwa yakivunjikavunjika yasipenye maji, na hilo lilifanya majengo yadumu kwa maelfu ya miaka.”

Ni “karatasi” ya namna gani iliyotumiwa wakati wa zamani?

Ulizo hilo linaulizwa kwa sababu Yohana, mumoja kati ya waandikaji wa Biblia, alisema hivi: “Ijapokuwa nina mambo mengi ya kuwaandikia ninyi, sitaki kufanya hivyo kwa karatasi na wino.”​—2 Yohana 12.

Neno la Kigiriki kharʹtes, linalotafsiriwa “karatasi,” linamaanisha karatasi iliyotengenezwa na papyrus (mumea ulio kama matete), ambao ni mumea unaokomaa mahali palipo na maji. Juu ya ufundi uliotumiwa ili kutengeneza karatasi za kuandikia kutokana na mumea huo, kitabu kimoja kinasema hivi: “Mimea hiyo ya papyrus ambayo inaweza kufikia urefu wa metre 3, ilimenywa na kukatwakatwa vipande​-vipande, ilipasuliwa na kutandazwa; kisha ilipigwapigwa na kipande cha muti upande huu na kugeuzwa upande mwengine na mwishowe chombo fulani kilitumiwa ili kuilainisha.”

Huko Misri na sehemu zilizo karibu na Bahari ya Chumvi, wachunguzi wa vitu vya zamani walivumbua maandishi mengi ya zamani yaliyoandikwa kwenye papyrus. Maandishi fulani yaliyopatikana katika maeneo hayo yaliandikwa wakati wa Yesu ao hata mbele ya hapo. Inawezekana maandishi fulani ya Biblia, kama vile barua zilizoandikwa na mitume, yaliandikwa kwanza kwenye papyrus.

[Maneno ili kueleza mahali picha zilitokea, ukurasa wa 11]

Spectrumphotofile/ photographersdirect.com

© FLPA/David Hosking/age fotostock