Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Kweli Miujiza Inafanyika?—Mambo Matatu Ambayo Watu Wengi Wanasema ili Kupinga Miujiza

Je, Kweli Miujiza Inafanyika?—Mambo Matatu Ambayo Watu Wengi Wanasema ili Kupinga Miujiza

Je, Kweli Miujiza Inafanyika?—Mambo Matatu Ambayo Watu Wengi Wanasema ili Kupinga Miujiza

JAMBO LA 1: Miujiza haifanyike kwa sababu inavunja sheria za asili. Yale tunayoelewa kuhusu sheria za asili yanategemea mambo ambayo wanasanyansi wamevumbua kutokana na mambo yanayotuzunguka. Lakini, sheria hizo zinafanana na sheria za luga fulani—kuna maneno fulani yasiyoheshimu sheria za luga. Uelewaji wetu wa “sheria” hizo za asili unaweza kuwa na mipaka. (Ayubu 38:4) Mwanasayansi mwenye bidii anaweza kupitisha maisha yake yote akijifunza sheria fulani ya asili. Lakini anapoona tu kitu kimoja kisichofuata sheria hiyo, mara moja anabadilisha maoni yake kuhusu sheria hiyo. Kwa hiyo, kutokujua jambo fulani hakumaanishe kwamba jambo linalojulikana si la kweli.

Historia fulani yenye kuchekesha inaonyesha kama ni vyepesi mutu kukataa ukweli kwa sababu hajue ukweli wote juu ya jambo linalozungumuziwa. John Locke (1632-1704) alieleza historia fulani inayomuhusu ambasadere wa Hollande na mufalme wa Siam (Thaïlande): Ambasadere huyo alipokuwa akimuelezea mufalme juu ya inchi yake, alimuambia kama wakati fulani iliwezekana tembo kutembea juu ya maji. Mufalme hakukubali wazo hilo na aliwaza kama ambasadere anamudanganya. Lakini, ambasadere huyo alikuwa tu anaeleza jambo fulani ambalo mufalme hakuwa anajua. Mufalme hakujua kama wakati maji yanaganda na kuwa barafu, tembo anaweza kutembea juu ya maji hayo. Mufalme aliona kama jambo hilo haliwezekane kwa sababu hakujua ukweli wote juu ya jambo hilo.

Ona mambo fulani yanayofanyika leo ambayo yalionekana kuwa hayawezekane miaka fulani iliyopita:

● Avion inaweza kubeba sasa watu zaidi ya 800 na kusafiri bila kutua kutoka muji wa New York mupaka Singapore, kwa mwendo wa kilometre 900 kwa saa.

● Kupitia video, watu kutoka sehemu mbalimbali za dunia wanaweza kufanya mikutano yao wakiwa wenye kuonana uso kwa uso.

● Maelfu ya nyimbo zinaweza sasa kuchungwa kwenye kitu kidogo sana ambacho hakifikie hata ukubwa wa kibweta cha kiberiti.

● Waganga wanaweza sasa kumupasua mutu na kumutia moyo wa mutu mwengine ao sehemu zingine za mwili.

Tunaweza kusema nini kutokana na mambo kama hayo? Tunaweza kusema hivi: Ikiwa watu wanaweza kufanya mambo ya ajabu ambayo hayakuwezekana katika miaka fulani iliyopita, basi kwa kweli Mungu aliyeumba ulimwengu na vitu vyote vilivyo ndani anaweza kufanya mambo ya ajabu sana ambayo hatuwezi kuelewa vizuri leo wala kufanya kama yeye. *​—Mwanzo 18:14; Mathayo 19:26.

JAMBO LA 2: Biblia inatumia miujiza ili kuchochea watu waiamini. Biblia haituambie tuamini miujiza yote. Na haituambie tusiamini miujiza. Biblia inatuonya tuwe waangalifu kuhusu miujiza na ishara za ajabu. Ona onyo hili lililo wazi: “Na yule mwovu atakuja kwa nguvu ya Shetani, na kufanya kila namna ya miujiza na ishara na maajabu ya uwongo, na kuleta kila namna ya udanganyifu wa uovu.”​—2 Wathesalonike 2:9, 10, Verbum Bible.

Yesu Kristo pia alisema kama wengi watajiita wafuasi wake lakini atawakataa kwa sababu wao si wafuasi wake wa kweli. Na hata wengine watamuambia hivi: “Bwana, Bwana, si tumehubiri neno la Mungu kwa jina lako? na kwa jina lako tumewafukuza mashetani? na kwa jina lako tumefanya miujiza mingi?” (Mathayo 7:22, Verbum Bible) Lakini Yesu alisema kama hatawakubali watu hao kuwa wafuasi wake. (Mathayo 7:23) Hilo linaonyesha wazi kama Yesu hakufundisha kwamba miujiza yote inatokana na Mungu.

Mungu hawaambie waabudu wake kama imani yao inapaswa kutegemea tu miujiza. Lakini, imani yao inapaswa kutegemea mambo ya kweli.​—Waebrania 11:1.

Kwa mufano, tuzungumuzie muujiza moja kati ya miujiza yenye kujulikana sana inayozungumuziwa katika Biblia, ni kusema, ufufuo wa Yesu Kristo. Miaka fulani kisha Yesu kufufuliwa, Wakristo fulani katika Korintho walianza kushakia ufufuo huo. Namna gani mutume Paulo aliwasaidia? Je, aliwaambia tu, “Muwe na imani zaidi?” Hapana. Ona namna alivyowakumbusha mambo yaliyotendeka. Alisema kama Yesu ‘alizikwa, ndiyo, . . . alifufuliwa siku ya tatu kulingana na Maandiko; na kwamba alimutokea Kefa, kisha wale kumi na wawili. Baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano wakati mumoja, ambao walio wengi kati yao wapo mupaka sasa.’​—1 Wakorintho 15:4-8.

Je, ilikuwa lazima Wakristo hao waamini muujiza huo? Paulo aliendelea kusema hivi: “Ikiwa Kristo hakufufuliwa, hakika kuhubiri kwetu ni bure, na imani yetu ni bure.” (1 Wakorintho 15:14) Paulo alichukua jambo hilo kwa uzito. Walipaswa kuamini kama Yesu alifufuliwa ao hakufufuliwa! Lakini Paulo alijua kama kwa kweli Yesu alifufuliwa, kwa sababu watu wengi waliojionea muujiza huo walikuwa wangali wazima wakati huo, na walieleza habari hiyo. Kwa kweli, watu hao waliojionea ufufuo wa Yesu walikuwa tayari kufa kuliko kukataa jambo walilojionea.​—1 Wakorintho 15:17-19.

JAMBO LA 3: Miujiza ni matukio ya kawaida ambayo watu ambao hawakusoma wanaelewa vibaya. Watu fulani waliosoma wanajaribu kueleza miujiza inayozungumuziwa katika Biblia kuwa matukio ya kawaida ambayo yalitukia bila nguvu za Mungu. Wanaona kama miujiza inayozungumuziwa katika Biblia ndiyo inafanya watu waamini habari zilizo ndani. Hata ikiwa miujiza fulani inayozungumuziwa katika Biblia kama vile matetemeko ya inchi, mapigo, na maporomoko ya udongo, ni mambo yaliyoweza kutokea kwa sababu ya nguvu fulani za asili—maelezo hayo ya watu wenye kusoma yanafanana katika jambo hili: Katika maelezo yao hawafikirie wakati ambapo miujiza hiyo inayozungumuziwa katika Biblia ilitokea.

Kwa mufano, watu wengine wamesema kama pigo la kwanza lililoletwa juu ya inchi ya Misri, ni kusema, kugeuzwa kwa Muto Nile kuwa damu, ilikuwa tu udongo mwekundu ndio ulichangana na maji ya Nile pamoja na viumbe fulani vyekundu vinavyoishi katika maji. Lakini, Biblia inasema kama muto huo uligeuzwa kuwa damu, si udongo mwekundu. Kuchunguza vizuri andiko la Kutoka 7:14-21 kunaonyesha kama muujiza huo ulitokea tu wakati Haruni alipiga fimbo juu ya Muto Nile, kufuatana na agizo la Musa. Hata ikiwa Muto Nile uligeuzwa kwa sababu ya tukio fulani la kawaida, muto haukujigeuza wenyewe, uligeuzwa tu wakati Haruni alipiga fimbo yake juu ya maji!

Mufano mwengine unaoonyesha kama ni jambo la lazima kufikiria wakati ambapo muujiza fulani ulitokea, ni jambo lililotokea wakati Waisraeli walikuwa karibu kuingia katika Inchi ya Ahadi. Hawangeweza kuvukia katika Inchi ya Ahadi kwa sababu Muto Yordani ulikuwa wenye kujaa. Biblia inatuambia jambo lililotokea. Inasema hivi: “Mara tu wachukuaji wa lile Sanduku walipofika Yordani na miguu ya makuhani waliolichukua Sanduku ilipotumbukizwa katika maji ya ukingoni . . . , ndipo maji yanayoshuka kutoka juu yakaanza kusimama. Yakasimama kama ukuta wa maji mbali sana huko Adamu, jiji lililo kando ya Sarethani.” (Yoshua 3:15, 16) Je, ni matetemeko ya inchi ao maporomoko ya udongo ndiyo yaliyotokeza jambo hilo? Biblia haiseme. Lakini muujiza huo ulitokea tu wakati makuhani walitumbukiza miguu yao katika maji. Na huo ndio wakati Yehova aliamuru muujiza huo utokee.​—Yoshua 3:7, 8, 13.

Kwa hiyo, je, hauone kama mambo hayo ilikuwa miujiza? Biblia inasema kama ilikuwa miujiza. Kupatana na yale Biblia inatuambia, mambo hayo hayakuwa tu matukio ya kawaida. Je, mutu mwenye akili anaweza kusema kama mambo hayo hayakutokea kwa sababu tu hayatokee kila siku?

[Maelezo ya chini]

^ Ikiwa una mashaka juu ya kuwapo kwa Mungu, tafazali usome broshua Je, Kweli Mungu Anatujali? na Uhai​—Ulitokana na Muumba? ao unaweza kumuona mutu aliyekupatia gazeti hili ili upate habari zingine.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Miaka fulani iliyopita, watu wengi hawakuwazia kama inawezekana kusafiri mamia ya kilometre kwa saa moja kwa njia ya avion