Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, imani ya kidini inasaidia watu kusahau magumu yao?

Je, imani ya kidini inasaidia watu kusahau magumu yao?

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Je, imani ya kidini inasaidia watu kusahau magumu yao?

▪ Watu fulani wanapopatwa na magumu, wanatumia vitu fulani vya kuwatuliza kwa muda; vitu hivyo vinawasaidia wasahau magumu yao na vinawazuia kuwaza kwa namna inayofaa. Kwa mufano, watu fulani wanatumia pombe ili kusahau magumu yao. Kwanza, pombe inaweza kuwasaidia wajitumainie zaidi na wajisikie kuwa na uwezo wa kupambana na magumu ya maisha. Lakini, kisha muda fulani wale wanaotumia pombe ili kusahau magumu yao wanajiletea matokeo mabaya. Basi tuseme nini juu ya imani ya kidini, je, inasaidia watu kusahau magumu yao?

Watu fulani wanawaza kama imani ni kukubali kila jambo bila kufikiri. Wanasema kama watu walio na imani hawawezi kutumia uwezo wao wa kufikiri ao kukubali mambo yenye kusadikisha yabadilishe imani yao. Watu kama hao wanasema kwamba imani yenye nguvu inasaidia watu kusahau magumu yao.

Biblia inasema mambo mengi juu ya imani. Lakini hakuna mahali popote ambapo inatutia moyo tuamini kila jambo bila kufikiri ao bila uhakikisho. Inatutia moyo tutumie uwezo wetu wa kufikiri. Inaonyesha kama watu wanaoamini kila neno hawana uzoefu, na hata ni wapumbavu. (Methali 14:15, 18) Kwa kweli, ni upumbavu kabisa kukubali kama wazo fulani ni la kweli bila kulichunguza! Kufanya hivyo ni kama kujaribu kuvuka barabara yenye motokari nyingi tukiwa wenye kufunga macho, kwa sababu tu mutu fulani anatuomba tufanye hivyo.

Kuliko kututia moyo tuamini kila jambo, Biblia inatuomba tufungue macho yetu ya mufano ili tusidanganywe. (Mathayo 16:6) Tunafungua macho yetu ya mufano tunapotumia ‘nguvu zetu za kufikiri.’ (Waroma 12:1) Biblia inatuzoeza kufikiri juu ya mambo yaliyo hakika na kuchukua maamuzi yenye kufaa yanayotegemea mambo ya kweli. Tuchunguze mifano fulani katika maandishi ya mutume Paulo.

Paulo alipowaandikia Wakristo wa kutaniko la Roma, hakutaka wamuamini Mungu kwa sababu tu aliwaambia wafanye hivyo. Lakini aliwatia moyo wachunguze mambo yanayohakikisha kama Mungu iko. Aliwaandikia hivi: “Sifa [za Mungu] ambazo hazionekani, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa, yaani, nguvu zake za milele na Uungu, hivi kwamba [wale wanaokataa nguvu za Mungu] hawana sababu ya kujitetea.” (Waroma 1:20) Paulo alitumia mawazo hayo hayo alipowaandikia Waebrania. Aliwaambia hivi: ‘Bila shaka, kila nyumba inajengwa na mutu fulani, lakini yeye aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.’ (Waebrania 3:4) Alipowaandikia Wakristo wa kutaniko la Thesalonike, aliwatia moyo wasiamini kila jambo. Alitaka ‘wahakikishe mambo yote.’​—1 Wathesalonike 5:21.

Imani ya kidini isiyotegemea mambo yaliyo hakika inaweza kumudanganya mutu na kumuletea matokeo mabaya. Juu ya imani ya kidini ya watu fulani wa wakati wake, Paulo aliandika hivi: “Nawatolea ushahidi kwamba wana bidii kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi.” (Waroma 10:2) Kwa hiyo, ni jambo la lazima kabisa kufuata shauri ambalo mutume Paulo aliwapatia Wakristo wa kutaniko la Roma. Aliwashauria hivi: ‘Mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mujihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.’ (Waroma 12:2) Imani inayotegemea ujuzi sahihi juu ya Mungu haitudanganye, lakini inakuwa “ngao kubwa” inayotulinda kiroho na kutusaidia kuwa na moyo mutulivu.​—Waefeso 6:16.

[Picha katika ukurasa wa 23]

Imani inaweza kuwa ngao inayotulinda