Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulizo la 1: Je, Maisha Yangu Yana Kusudi?

Ulizo la 1: Je, Maisha Yangu Yana Kusudi?

Ulizo la 1: Je, Maisha Yangu Yana Kusudi?

ROSALIND, aliyekomalia huko Angleterre, alipenda kujua mambo mengi sana. Tena, alipenda kusaidia watu, kwa hiyo, alipomaliza masomo alipata kazi ya kusaidia watu wasio na makao, walemavu na watu walio na matatizo ya kujifunza. Hata kama alikuwa na kazi nzuri na mali nyingi, anasema hivi: “Kwa miaka mingi nilijiuliza, ‘Sababu gani tunaishi?’ na ‘Maisha yana kusudi gani?’”

Sababu gani tunajiuliza ulizo hilo? Kwa sababu sisi ni tofauti na wanyama ambao hawana akili. Tuna uwezo wa kujifunza kutokana na mambo ya zamani, kupanga mambo ya wakati unaokuja, na kutafuta kusudi katika maisha yetu.

Watu fulani wamejibu ulizo hilo namna gani? Watu wengi wanawaza kama kusudi kubwa la maisha ni kupata mali nyingi ao kujulikana sana ili kuwa na furaha.

Jibu hilo linaonyesha nini? Linaonyesha mambo ambayo watu wanatia pa nafasi ya kwanza katika maisha yao. Tamaa zao ndizo za maana zaidi kuliko kufanya mapenzi ya Mungu.

Biblia inafundisha nini? Mufalme Sulemani alijirundikia mali nyingi sana na kufuatia raha lakini aliona kama mambo hayo hayakumuwezesha kupata kusudi katika maisha. Alivumbua jambo linalomufanya mutu awe na kusudi katika maisha. Aliandika hivi: ‘Huu ndio mwisho wa mambo, kila jambo limekwisha sikiwa: Muogope Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwa maana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu.’ (Mhubiri 12:13) Kushika amri za Mungu kunatia ndani nini?

Mungu anakusudia pia tufurahie maisha. Sulemani aliandika hivi: ‘Kwa mwanadamu hakuna jambo bora kuliko kwamba ale, naam, anywe na kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya kazi yake ngumu. Hilo pia mimi nimeliona, naam mimi, ya kwamba linatoka kwenye mukono wa Mungu wa kweli.’​—Mhubiri 2:24.

Tena Mungu anataka tuwapende watu wa familia yetu na kuwahangaikia. Ona mashauri yenye kufaa na mepesi kufuata ambayo anatolea kila mutu wa familia.

‘Waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.’​—Waefeso 5:28.

‘Muke anapaswa kumuheshimu sana mume wake.’​—Waefeso 5:33.

‘Enyi watoto, muwatii wazazi wenu.’​—Waefeso 6:1.

Ikiwa tunatumikisha mashauri hayo ya Biblia, tutapata furaha na tutatosheka. Lakini, jambo la lazima zaidi tunaloweza kufanya ni kujifunza yote tunayoweza juu ya Muumbaji wetu na kumufanya kuwa Rafiki yetu. Kwa hiyo, Biblia inatuomba ‘tumukaribie Mungu.’ Kisha inatuahidi hivi: “Naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8) Ukimukaribia Mungu, maisha yako yatakuwa na kusudi.

Rosalind, aliyetajwa mwanzoni mwa habari hii, anaona kama sasa maisha yake yana kusudi. Ili kujua kile kilichomusaidia, usome ukurasa wa 10 wa gazeti hili.

Ili kujua mengi juu ya namna unavyoweza kuishi maisha yanayomupendeza Mungu, usome sura ya 12 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Unaweza pia kupakua kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.mt1130.com

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Yesu Alifundisha Nini juu ya Kusudi la Maisha?

Yesu alijua vizuri kusudi la maisha yake. Alisema hivi: “Kwa ajili ya hili mimi nimezaliwa, na kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli.” (Yohana 18:37) Yesu alipitisha maisha yake akifundisha watu kweli juu ya Mungu na juu ya mambo ambayo anakusudia kufanya.

Maisha yetu yatakuwa na kusudi ikiwa tunafuata mufano wa Yesu. Ndiyo sababu Yesu aliwaomba watu wajifunze kutoka kwake. (Mathayo 11:29) Tuchunguze tu njia mbili zinazoweza kutusaidia kufanya hivyo.

Yesu alifundisha kama ili tuwe na furaha, tunapaswa ‘kutambua uhitaji wetu wa kiroho.’ (Mathayo 5:3) Tunaweza kutosheleza mahitaji yetu ya kiroho ikiwa tunaendelea kujifunza juu ya ‘Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule aliyetuma, Yesu Kristo.’—Yohana 17:3.

Yesu aliwaamuru wafuasi wake wawafundishe wengine mambo waliyojifunza. Alisema hivi: ‘Kwa hiyo nendeni mukafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mukiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.’—Mathayo 28:19, 20.

Wale wanaotosheleza mahitaji yao ya kiroho kwa kujifunza Biblia na kutumikisha mambo wanayojifunza, wanatambua kama maisha yao yanabadilika na kuwa mazuri. Wanasadikishwa zaidi kama maisha yao yana kusudi kabisa wanapoanza kuwafundisha wengine juu ya Mungu.