Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | LIES THAT MAKE GOD SEEM UNLOVABLE

Fundisho la Uongo Ambalo Limemufanya Mungu Kuwa Asiye na Huruma

Fundisho la Uongo Ambalo Limemufanya Mungu Kuwa Asiye na Huruma

MAMBO AMBAYO WATU WENGI WANAAMINI:

“Kisha tu kifo, nafsi za watu ambao wanakufa katika hali ya zambi zinashuka katika helo, mahali ambapo zinateswa kwa kuazibiwa katika moto wa mateso, ‘moto wa milele.’” (Catechism of the Catholic Church) Viongozi fulani wa kidini wanasema kwamba helo ni hali ya kutengwa kabisa na Mungu.

KWELI YA BIBLIA:

‘Nafsi inayotenda zambi​—hiyo yenyewe itakufa.’ (Ezekieli 18:4) Wafu “hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5) Ikiwa nafsi inakufa na haijui lolote, namna gani inaweza kuteseka katika “moto wa milele” ao hata kuteseka kwa kutengwa milele na Mungu?

Katika Biblia, neno la Kiebrania na la Kigiriki ambalo mara nyingi linatafsiriwa “helo” linamaanisha tu kaburi. Kwa mufano, wakati Ayubu alisumbuliwa na ugonjwa mubaya sana, alisali hivi: “Laiti ungenificha katika Kaburi [“katika kuzimu,” Union Version].” (Ayubu 14:13) Ayubu alitaka kupumuzika, si katika mahali pa mateso ao palipotengwa na Mungu, lakini katika kaburi.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Fundisho la moto wa mateso linawafanya watu wasimupende Mungu na wasimukaribie. Rocío, ambaye anaishi Mexico anasema hivi: “Tangu nilipokuwa mutoto nilifundishwa fundisho la moto wa mateso. Niliogopa sana hivi kwamba sikuwazia kuwa Mungu alikuwa na sifa nzuri yoyote. Nilifikiri kwamba alikuwa mwenye hasira na asiyevumilia chochote.”

Mambo ambayo Biblia inaeleza waziwazi juu ya hukumu za Mungu na hali ya wafu yalibadilisha maoni ya Rocío juu ya Mungu. Anasema tena hivi: “Nilijisikia niko huru kwa sababu muzigo muzito niliokuwa nao moyoni ulikuwa umeondolewa juu yangu. Nilianza kuamini kwamba Mungu anatutakia mema, anatupenda, na kwamba ninaweza kumupenda. Yeye ni kama baba ambaye anawashika watoto wake kwenye mikono na ambaye anawatakia mema.”​—Isaya 41:13.

Watu wengi wamejikaza sana kumutii Mungu kwa sababu wanaogopa moto wa mateso, lakini Mungu hataki umutumikie kwa sababu unamuogopa. Yesu alisema hivi: ‘Lazima umupende Yehova Mungu wako.’ (Marko 12:29, 30) Zaidi ya hilo, wakati tunatambua kwamba leo Mungu hatendi isivyo haki, tunaweza kutumainia kwamba hukumu zake za wakati unaokuja zitakuwa za haki pia. Kama Elihu, rafiki ya Ayubu, tunaweza kusema hivi kwa uhakika: “Ndiyo, kwa kweli, Mungu hatendi kwa uovu, na Mweza​-Yote hapotoshi hukumu.”​—Ayubu 34:12.