Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Ni nini inayochochea watu wengi wafikirie ikiwa kuna Muumbaji?

Uzima ni jambo la ajabu, sivyo?

Miaka 3000 hivi iliyopita, muandikaji wa mashairi ao maandishi yaliyopangwa kwa utaratibu fulani aliandika hivi: “Nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha.” (Zaburi 139:14) Unapofikiria namna mutoto anakomaa kutokana na chembe moja, hilo halikushangaze sana? Watu wengi wanaamini kuwa vitu vilivyo na uzima viliumbwa na Muumbaji.—Soma Zaburi 139:13-17; Waebrania 3:4.

Yule aliyeumba ulimwengu na kufanya dunia iikaliwe ndiye aliumba pia uzima. (Zaburi 36:9) Amezungumuza na watu na ametuambia juu yake mwenyewe.—Soma Isaya 45:18.

Tulitokana na wanyama?

Katika mambo mengi, miili yetu inafanana na miili ya wanyama. Lakini hilo ni kwa sababu watu na wanyama waliumbwa na Muumbaji ili waishi kwenye dunia. Aliumba mutu wa kwanza kutokana na mavumbi, lakini haiko kutokana na munyama.—Soma Mwanzo 1:24; 2:7.

Watu wako tofauti na wanyama katika mambo mbili ya maana. Jambo la kwanza, watu wana uwezo wa kujua Muumbaji, kumupenda, na kumuheshimu. Jambo la pili, watu waliumbwa ili waishi milele lakini hapana wanyama. Hata hivyo leo, watu wote wanariti kifo kwa sababu mutu wa kwanza alikataa kuongozwa na Muumbaji.—Soma Mwanzo 1:27; 2:15-17.