Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Kusudi la maisha ni nini?

wakati fulani unaona kuwa maisha ni mafupi sana?

Umekwisha kujiuliza ikiwa kusudi tu la maisha ni kucheza, kufanya kazi, kuoa, kuwa na familia, na kuzeeka? (Ayubu 14:1, 2) Biblia inaonyesha kama hata watu wenye hekima wamejiuliza juu ya jambo hilo.—Soma Mhubiri 2:11.

Maisha iko na maana fulani? Kwanza, tunapaswa kujiuliza, Maisha yalianza namna gani? Kisha kuchunguza namna ubongo wetu na sehemu zingine za mwili wetu zimeumbwa, watu wengi wamefikia kusema kuwa tuliumbwa na Muumbaji mwenye hekima. (Soma Zaburi 139:14.) Kama ni hivyo, Muumbaji huyo alituumba kwa sababu fulani! Kujua sababu hiyo kunaweza kufanya maisha yetu yakuwe na maana zaidi.

Sababu gani watu waliumbwa?

Mungu alibariki mwanaume na mwanamuke wa kwanza na akawapatia kazi yenye kufurahisha. Kusudi lake lilikuwa kwamba wajaze dunia, waifanye kuwa paradiso, na waishi milele.—Soma Mwanzo 1:28, 31.

Kusudi la Mungu halikutimia kwa sababu watu walipinga utawala wake. Lakini Mungu hakutuachilia, na hakubadilisha kusudi lake juu yetu na juu ya dunia. Biblia inatuhakikishia kama Mungu amefanya mipango ili kuokoa watu waaminifu na kama kusudi lake juu ya dunia litatimia! Kwa hiyo, Mungu anapenda ukuwe na maisha yenye alikusudia! (Soma Zaburi 37:29.) Ujifunze kupitia Biblia namna unaweza kupata faida kutokana na kusudi hilo la Mungu.