Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | WATU WALIOKUFA—WANAWEZA KUISHI TENA?

Kuko Tumaini kwa Ajili ya Watu Waliokufa?

Kuko Tumaini kwa Ajili ya Watu Waliokufa?

Watu waliokufa wanaweza kuishi tena?

JIBU LA BIBLIA: ‘Saa inakuja ambayo wale wote walio ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti [ya Yesu] na kutoka.’—Yohana 5:28, 29.

Kwa kusema hivyo, Yesu alitabiri kuwa wakati unaokuja, chini ya uongozi wa Ufalme wake, Kaburi litabakia wazi. Fernando, mwenye tulizungumuzia katika habari yenye kutangulia, anakumbuka hivi: “Nilishangaa wakati nilisoma mara ya kwanza Yohana 5:28, 29. Andiko hilo lilinipatia tumaini la kweli, na nikakuwa na mawazo ya muzuri juu ya wakati unaokuja.”

Wakati wa zamani, mwanaume muaminifu Ayubu alitumaini kama Mungu angemufufua. Ayubu aliuliza hivi: ‘Mutu akikufa, anaweza kuishi tena?’ Kisha alijibu hivi kwa uhakika: ‘Mimi nitangojea siku zote za kazi yangu ya kulazimishwa [wakati angekuwa katika Kaburi], mupaka kitulizo changu kikuje. Wewe utaita, na mimi mwenyewe nitakujibu.’—Ayubu 14:14, 15.

Ufufuo wa Lazaro unatupatia tumaini la wakati unaokuja

Wazo la ufufuo halikukuwa mupya kwa Martha, dada ya Lazaro. Kisha Lazaro kufa, Yesu alimuambia Martha hivi: “Ndugu yako atafufuka.” Martha alijibu hivi: “Ninajua atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.” Kisha Yesu akamuambia: ‘Mimi ndiye ufufuo na uzima. Yule anayeniamini, hata akikufa, atarudi kwenye uzima.’ (Yohana 11:23-25) Kisha, Yesu akamufufua Lazaro bila kukawia! Habari hiyo yenye kufurahisha inatuonyesha mambo makubwa yenye yatafanyika wakati unaokuja. Wazia ufufuo kama huo unafanyika katika dunia yote!

Watu fulani watafufuliwa ili kuishi mbinguni?

JIBU LA BIBLIA: Neno la Mungu linaonyesha kama ufufuo wa Yesu ulikuwa tofauti na ufufuo mbalimbali munane unaozungumuziwa katika Biblia. Watu hao munane walifufuliwa na kuishi tena duniani. Lakini, juu ya ufufuo wa Yesu, Biblia inasema hivi: ‘Yesu Kristo . . . iko [kwenye] mukono wa kuume wa Mungu, kwa maana alienda zake mbinguni.’ (1 Petro 3:21, 22) Ni Yesu tu ndiye angefufuliwa ili kwenda mbinguni? Yesu alikuwa amewaambia mitume wake hivi: “Nikienda na kuwatayarishia ninyi mahali, nitakuja tena nami nitawapokea ninyi nyumbani kwangu mwenyewe, ili mahali nilipo mimi, ninyi pia muwe hapo.”—Yohana 14:3.

Kristo alienda mbinguni na alitayarisha kuja kwa wanafunzi wake fulani. Watu wenye kufufuliwa ili kwenda mbinguni watafikia hesabu ya watu 144000. (Ufunuo 14:1, 3) Lakini wanafunzi hao wa Yesu wataenda kufanya nini mbinguni?

Watakuwa na kazi nyingi! Maandiko yanasema hivi: ‘Mwenye furaha na mutakatifu ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; kifo cha pili hakina mamlaka juu ya hao, bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.’ (Ufunuo 20:6) Watu hao wenye kufufuliwa ili kwenda mbinguni watatawala pamoja na Kristo; watakuwa wafalme na makuhani juu ya dunia.

Ni nani wengine watafufuliwa?

JIBU LA BIBLIA: Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu yanazungumuzia hotuba hii ya mutume Paulo: “Nami nina tumaini kwa Mungu, tumaini ambalo watu hawa pia wanalo, kwamba kutakuwa na ufufuo wa waadilifu [wenye haki] na wasio waadilifu pia.”—Matendo 24:15.

Neno la Mungu linatupatia uhakika kuwa watu wengi sana waliokufa wataishi tena

Ni nani watakuwa kati ya “waadilifu” wenye Paulo anazungumuzia? Ona mufano moja. Mungu alimuambia mwanaume muaminifu Danieli hivi wakati alikaribia kufa: “Utapumzika, lakini utasimama kwa ajili ya fungu lako mwishoni mwa zile siku.” (Danieli 12:13) Danieli ataamuka kutoka katika kifo ili kuishi wapi? “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” (Zaburi 37:29) Na Yesu alitabiri hivi: ‘Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watairiti dunia.’ (Mathayo 5:5) Danieli na wanaume na wanawake wengine waaminifu watafufuliwa ili kuishi tena duniani, hata milele.

Ni nani watakuwa kati ya “wasio waadilifu” wenye Paulo anazungumuzia? Ni watu wengi sana wenye waliishi na kufa, wengi kati yao hawakupata hata nafasi ya kuelewa na kutumia mafundisho ya Biblia. Kisha kufufuliwa kwao, watapata nafasi ya kujua Yehova * na Yesu na kuwapenda. (Yohana 17:3) Watu wote wenye kuchagua kumutumikia Mungu watakuwa na tumaini la kuishi milele kama vile Yehova anaishi.

Watu wote wenye kuchagua kumutumikia Mungu watakuwa na tumaini la kuishi milele katika furaha na afya ya muzuri kabisa

Hali ya maisha itakuwa namna gani katika dunia?

JIBU LA BIBLIA: Mungu “atafuta [atapanguza] kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Ufunuo 21:4) “Na hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.”—Isaya 65:21.

Wazia unaishi katika hali kama hizo pamoja na watu wenye unapenda ambao watakuwa wamefufuliwa! Lakini ulizo lenye kubaki ni hili, Namna gani unaweza kuwa hakika kama kutakuwa ufufuo?

^ fu. 15 Biblia inaonyesha kuwa jina la Mungu ni Yehova.