Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Masimulizi Kuhusu Maisha Ya Watu

Nimepata Jambo la Muzuri Zaidi Kuliko Kujulikana Sana

Nimepata Jambo la Muzuri Zaidi Kuliko Kujulikana Sana

Siku moja usiku katika mwaka wa 1984, maisha yangu yalibadilika. Nilikuwa kijana wa kawaida tu lakini nikakuwa mutu mwenye kujulikana sana. Picha yangu ilikuwa kwenye ukurasa wa kwanza wa magazeti. Nilikuwa ninaimba, nilikuwa ninacheza, nilitoa hotuba mbalimbali, nilisimamia maonyesho kwenye TV, nilikuwa ninavaa nguo za muzuri, na nilikuwa ninaonekana pamoja na watu wa maana, kama vile gavana wa Hong Kong.

Mwaka wenye ulifuata, nilianza kucheza katika filme mbalimbali, mara nyingi nilikuwa muchezaji mukubwa katika filme hizo. Waandishi wa habari walitaka kupata habari juu ya maisha yangu, wapiga-picha walitaka kupata picha yangu, na watu walitaka nikuwe wakati filme zinaonyeshwa kwa mara ya kwanza, nikuwe nafasi kwenye watu wanafungua majengo mapya ili nikate kamba ya kufungua, nikuwe kwenye vyakula vya muchana na vya mangaribi. Sikuzote, nilivutia uangalifu wa watu.

Ninacheza filme yenye kuonyesha mambo ya hatari

Lakini pole kwa pole, niliona kuwa mambo hayo yote hayakukuwa yenye kuvutia kama vile nilikuwa ninawaza. Nilikuwa ninacheza sana katika filme zenye kuonyesha mambo ya hatari. Mara nyingi, wachezaji wa Hong Kong hawakutumia watu wengine ili kucheza mahali pao katika sehemu hatari kama vile wachezaji wa Hollywood walikuwa wanafanya, kwa hiyo mimi mwenyewe nilicheza sehemu zenye kuwa hatari, kama vile kutembeza pikipiki juu ya motokari. Filme nyingi zenye nilicheza zilikuwa zenye kuonyesha uasherati na jeuri, zingine zilionyesha mambo ya mashetani.

Katika mwaka wa 1995, niliolewa na mwanaume fulani mwenye alikuwa anafanya filme. Hata kama nilionekana kuwa na kila kitu chenye kinaweza kuniletea furaha, ni kusema, kujulikana, utajiri, na bwana mwenye kunipenda, nilikuwa mwenye kushuka moyo na mwenye huzuni. Niliamua kuacha kazi ya kucheza filme.

NILIKUMBUKA IMANI YANGU YA WAKATI NILIKUWA MUTOTO

Nilianza kukumbuka kwa furaha imani yangu ya wakati nilikuwa mutoto mudogo. Wakati huo, kila Siku ya Sita mimi na dada yangu tulikuwa tunaenda kutembelea familia moja ya Mashahidi wa Yehova. Joe McGrath, baba wa familia hiyo, alikuwa anatufundisha Biblia sisi pamoja na watoto wake watatu wanawake. Familia yao ilikuwa yenye furaha na yenye upendo. “Papa Joe” alikuwa anatendea bibi yake na watoto wake kwa heshima. Tena, nilifurahia kuenda nao kwenye mikutano yao ya Kikristo. Wakati fulani tulienda kwenye mikusanyiko mikubwa. Vipindi hivyo vilikuwa vya furaha. Wakati nilikuwa pamoja na Mashahidi wa Yehova nilijisikia salama.

Lakini, mambo yenye kuhuzunisha yalinifikia katika familia yetu. Tabia za baba yangu ziliumiza mama yangu, na mama akakuwa mwenye kushuka moyo sana. Wakati nilikuwa na miaka karibu 10, mama yangu aliacha kujiunga na Mashahidi wa Yehova. Niliendelea lakini haiko kwa moyo wote na nikabatizwa wakati nilikuwa na miaka 17. Lakini, muda mufupi kisha hapo, nilianza kuwa na tabia zisizokuwa za Kikristo, na sikukuwa tena mushiriki wa kutaniko.

NILIAMUA KURUDIA

Muda mufupi kisha ndoa yangu, wazee wawili wa kutaniko la Mashahidi wa Yehova la eneo letu walikuja kunitembelea. Walinifasiria namna ninaweza kumurudilia Yehova Mungu, na wakafanya mupango ili misionere mumoja mwenye kuitwa Cindy anisaidie. Wakati huo, nilikuwa nimepoteza imani yangu kwa kiasi kikubwa, kwa hiyo, nilimuambia anihakikishie kuwa Biblia ni Neno la Mungu kabisa. Alinionyesha mifano ya unabii mbalimbali wa Biblia wenye ulikuwa umetimia. Pole kwa pole, tulifikia kuwa marafiki wa sana, na alinitia moyo nijifunze pamoja naye mafundisho ya musingi ya Biblia, na nikakubali kufanya hivyo. Kwa mara ya kwanza nilifikia kumuona Yehova kuwa Mungu mwenye upendo, mwenye anataka nikuwe na furaha.

Nilipoanza tena kuenda kwenye mikutano ya Kikristo, nilitambua kama nilijisikia kuwa mwenye furaha zaidi wakati nilikuwa pamoja na Mashahidi wa Yehova kuliko wakati nilikuwa na watu wenye nilitumika nao katika kazi yangu ya kucheza filme. Lakini mambo yenye yalinifikia nilipokuwa mutoto yalifanya nijisikie kuwa siwezi kuaminia mutu yeyote, na mimi mwenyewe sikujipenda. Dada fulani katika kutaniko alinisaidia wakati alinionyesha katika Biblia namna ya kupambana na mawazo hayo ya moyoni, na tena nilijifunza namna ya kuwa na marafiki wazuri.

JAMBO FULANI LA MUZURI ZAIDI KULIKO KUJULIKANA SANA

Katika mwaka wa 1997, mimi na bwana yangu tulihamia Hollywood, Kalifornia, katika inchi ya Amerika. Huko nilitumia wakati mwingi ili kusaidia watu wapate faida ya hekima yenye kuwa katika Neno la Mungu. Kufundisha watu kumenipatia furaha nyingi zaidi kuliko kujulikana kwa sababu ya kucheza filme. Kwa mufano, katika mwaka 2002, nilikutana na Cheri, rafiki yangu wa zamani wa Hong Kong. Maisha yake na maisha yangu yalifanana kwa njia nyingi. Ni yeye alichaguliwa kuwa Miss wa Hong Kong mwaka moja mbele yangu. Wakati nilichaguliwa kuwa Miss, yeye ndiye alinivalisha taji (couronne). Yeye pia alikuwa muchezaji wa filme, kisha akakuwa mutu mwenye kufanya filme, na alitumika na wasimamizi wenye kujulikana sana. Na yeye alikuwa amehamia Hollywood.

Nilimusikilia Cheri huruma wakati nilijua kama muchumba wake alikuwa amekufa kwa sababu ya mshituko wa moyo. Hakuweza kupata jambo la kumutia moyo katika dini yake ya Buda. Kama mimi, alikuwa amejulikana sana; hilo ni jambo lenye watu wengine wanatamani. Lakini alikuwa mwenye huzuni na hakuweza kuaminia mutu yeyote. Nilianza kuzungumuza naye mambo yenye nilikuwa nimejifunza katika Biblia, lakini kwa sababu ya dini yake ya Buda, ilikuwa vigumu kwake kupendezwa na mambo hayo.

Rafiki yangu Cheri mahali pa kuchezea filme

Siku moja katika mwaka wa 2003, Cheri aliniita kwenye telefone wakati alikuwa katika muji wa Vancouver, Kanada, kwenye alikuwa anafanya filme. Kwa furaha, aliniambia kama alikuwa anatembeza motokari yake na kufurahia eneo la mashamba, na mara moja akaanza kusali hivi kwa sauti kubwa: “Uniambie, Mungu wa kweli ni nani? Jina lako ni nani?” Wakati huo, alipita na motokari yake karibu na Jumba la Ufalme na kuona jina Yehova. Aliona kuwa hilo lilikuwa jibu kutoka kwa Mungu, na alitaka kukutana na Mashahidi wa Yehova bila kukawia. Nilifanya mipango, na kisha siku kidogo, alienda kwenye mikutano katika kutaniko la luga ya Kichina katika muji wa Vancouver.

Kisha Cheri aliniambia hivi: “Watu hawa wanapendezwa na mimi kabisa. Ninaweza kuwaambia namna ninajisikia.” Nilifurahi sana kusikia hivyo, kwa sababu Cheri hakujifanyia marafiki wakati alikuwa katika kazi ya kufanya filme. Cheri aliendelea kukusanyika. Lakini, katika mwaka wa 2005, alifanya mapatano ya kutokeza filme mbili ndefu katika China, kwa hiyo ilikuwa lazima arudie Hong Kong. Jambo la kufurahisha ni kwamba, katika mwaka wa 2006, Cheri alijitoa kwa Yehova na akabatizwa kwenye mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika muji wa Hong Kong. Hata kama alipenda kutumikia Yehova zaidi, kazi yake ya kufanya filme ilifanya ikuwe vigumu, na hakukuwa mwenye furaha.

FURAHA YA KUSAIDIA WENGINE

Katika mwaka wa 2009, maisha ya Cheri yalibadilika sana. Aliamua kuachana na kazi ya kufanya filme ili kutumikia Yehova zaidi. Alijifanyia marafiki wengi wapya katika kutaniko la Kikristo. Akakuwa muhubiri wa wakati wote wa habari njema ya Ufalme na alifurahi kabisa kusaidia watu kupata maisha ya muzuri.—Mathayo 24:14.

Kisha Cheri aliamua kujifunza Kinepali ili kuunga mukono kikundi kidogo cha Kinepali katika muji wa Hong Kong. Katika muji wa Hong Kong, Wanepali wengi wanapuuzwa ao hata kuzarauliwa kwa sababu hawazungumuze muzuri Kiingereza ao Kichina, na kwa sababu wako na desturi tofauti. Cheri aliniambia namna alifurahia sana kusaidia watu hao kuelewa Biblia. Kwa mufano, siku moja wakati alikuwa anahubiri nyumba kwa nyumba, alikutana na mwanamuke mumoja Munepali mwenye alikuwa anajua mambo kidogo tu juu ya Yesu lakini hakukuwa anajua jambo lolote juu ya Yehova, Mungu wa kweli. Cheri alitumia Biblia ili kumuonyesha kama Yesu alisali kwa Baba yake wa mbinguni. Wakati mwanamuke huyo alijua kama anaweza kusali kwa Mungu wa kweli anayeitwa Yehova, alikubali kujifunza Biblia. Bila kukawia, bwana yake na mutoto wake mwanamuke walianza pia kujifunza Biblia.—Zaburi 83:18; Luka 22:41, 42.

Cheri leo

Wakati niliona kama Cheri alifurahia sana kuwa muhubiri wa wakati wote, nilijiuliza, ‘Ni jambo gani linanizuia kufanya hivyo pia?’ Wakati huo, mimi pia nilikuwa ninaishi tena Hong Kong. Niliamua kupanga mambo muzuri katika maisha yangu ili niweze kutumia wakati mwingi katika kazi ya kufundisha watu kweli ya Biblia. Nimetambua kuwa kusikiliza watu na kuwasaidia kuelewa Neno la Mungu kunaniletea furaha ya kweli.

Nimetambua kuwa kusaidia watu kuelewa Neno la Mungu kunaniletea furaha ya kweli

Kwa mufano, nimeweza kujifunza Biblia na mwanamuke mumoja Muvietnamu mwenye sikuzote alikuwa na huzuni na mara nyingi alikuwa na machozi katika macho yake. Sasa iko na mawazo ya muzuri juu ya maisha na anafurahia kabisa kujiunga na kutaniko.

Mimi na Cheri tulipata jambo la muzuri zaidi kuliko kujulikana. Hata kama mambo ya filme yalipendeza na yalifanya tujulikane, kufundisha watu juu ya Yehova Mungu kunafanya tukuwe na furaha zaidi kwa sababu kunamuletea utukufu. Tumejionea kuwa maneno haya ya Yesu ni ya kweli kabisa: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.