Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MUNGU ANAONA VITA NAMNA GANI?

Namna Mungu Aliona Vita Wakati wa Mitume

Namna Mungu Aliona Vita Wakati wa Mitume

Watu walikuwa wanaonewa. Kama wazazi wao wa zamani, Wayahudi wenye waliishi wakati wa mitume walisali tena na tena kwa Mungu ili awasaidie, lakini sasa ilikuwa ili awatoshe katika mateso ya Utawala wa Roma wenye ulikuwa unawaonea. Kisha walisikia juu ya Yesu. Angehakikisha kama yeye ndiye Masiya aliyeahidiwa? Haishangaze kuona kama watu wengi ‘walitumainia kwamba mutu huyu ndiye angekomboa Israeli’ kutoka katika mateso ya Waroma wenye walikuwa wanawaonea. (Luka 24:21) Lakini hawakupata musaada wowote. Kuliko wapate musaada, majeshi ya Waroma yalikuja na kuharibisha Yerusalemu na hekalu lake katika mwaka wa 70 kisha kuzaliwa kwa Yesu.

Ni jambo gani lilitokea? Sababu gani Mungu hakupigania Wayahudi kama vile alifanya wakati wa zamani? Ao sababu gani hakuwaruhusu wapigane vita ili wajikomboe kutoka kwa watu wenye walikuwa wanawaonea? Mawazo ya Mungu juu ya vita yalikuwa yamebadilika? Hapana. Lakini, jambo fulani lilikuwa limebadilika sana juu ya Wayahudi. Walikuwa wamemukataa Yesu, Mwana wa Mungu, kuwa Masiya. (Matendo 2:36) Kwa hiyo, taifa lote lilipoteza urafiki wake wa pekee pamoja na Mungu.—Mathayo 23:37, 38.

Yehova hakulinda tena taifa la Wayahudi na Inchi yao ya Ahadi, na hata Wayahudi hawakukuwa tena na haki ya kusema kama wangepigana vita yenye Mungu alikubali ao yenye aliunga mukono. Kama vile Yesu alitabiri, baraka zenye kuletwa kwa sababu ya kukubaliwa na Mungu zilinyanganywa taifa la kimwili la Israeli na kupewa taifa jipya, ni kusema, taifa la kiroho lenye Biblia iliita baadaye “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16; Mathayo 21:43) Kutaniko la Wakristo watiwa-mafuta ndilo lilionekana kuwa Israeli la kiroho la Mungu. Katika siku za mitume waliambiwa waziwazi hivi: “Sasa ninyi ni watu wa Mungu.”—1 Petro 2:9, 10.

Kwa sababu Wakristo wa wakati wa mitume walikuwa sasa “watu wa Mungu,” Mungu aliwapigania ili Waroma wasiendelee kuwaonea? Ao aliwaruhusu wapigane vita na watu wenye walikuwa wanawaonea? Hapana, hakufanya hivyo. Sababu gani? Juu ya vita zenye Mungu anaomba zipiganwe, yeye mwenyewe anaamua ni wakati gani vita kama hizo zinapaswa kupiganwa, kama vile tuliona katika sehemu yenye ilitangulia. Mungu hakupigana vita kwa ajili ya Wakristo wa wakati wa mitume na hakuwaruhusu kupigana vita. Ni wazi kama wakati wa mitume haukukuwa wakati wa Mungu wa kupigana vita ili kumaliza ubaya na matendo ya kuonea wengine.

Kwa hiyo, kama vile watumishi wa Mungu wa zamani, Wakristo wa wakati wa mitume walipaswa kungoja mupaka wakati wa Mungu wa kumaliza ubaya na matendo ya kuonea wengine. Mbele wakati huo ufike, Mungu hakuwaruhusu wajiamulie kupigana vita na adui zao. Yesu Kristo alionyesha waziwazi jambo hilo katika mafundisho yake. Kwa mufano, hakuwaambia wanafunzi wake wapigane vita, lakini aliwaambia hivi: ‘Muendelee kuwapenda adui zenu na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa.’ (Mathayo 5:44) Wakati Yesu alitabiri kama muji wa Yerusalemu ungeshambuliwa na majeshi ya Waroma katika siku za mitume, hakuambia wanafunzi wake wabakie na wapigane vita, lakini aliwaambia wakimbie; na wanafunzi wake walifanya hivyo.—Luka 21:20, 21.

Tena, mutume Paulo mwenye aliongozwa na roho ya Mungu, aliandika hivi: ‘Musijilipizie kisasi, . . . kwa maana imeandikwa: Kisasi ni changu; mimi nitalipa, asema Yehova.’ (Waroma 12:19) Paulo alikuwa anataja maneno yenye Mungu alisema miaka mingi mbele ya hapo. Maneno hayo yanapatikana katika andiko la Mambo ya Walawi 19:18 na Kumbukumbu la Torati 32:35. Kama vile tuliona katika sehemu yenye ilitangulia, njia moja yenye Mungu alitumia ili kulipizia watu wake kisasi ilikuwa ni kuwasaidia kupigana vita na maadui wao. Kwa hiyo, maneno ya Paulo yanaonyesha kama mawazo ya Mungu juu ya vita yalikuwa hayajabadilika. Wakati wa mitume, Mungu aliendelea kuona vita kuwa njia ya haki ya kulipizia watu wake kisasi na kumaliza aina mbalimbali ya matendo ya kuonea wengine na ya ubaya. Hata hivyo, kama vile ilikuwa zamani, ni Mungu mwenyewe aliamua ni wakati gani vita kama hizo zilipaswa kupiganwa na ni nani alipaswa kupigana.

Ni wazi kama Mungu hakuruhusu Wakristo wa wakati wa mitume wapigane vita. Lakini tuseme nini juu ya leo? Mungu ameruhusu kikundi fulani cha watu kipigane vita leo? Ao huu ndio wakati wa Mungu wa kuchukua hatua na kupigana vita kwa ajili ya watumishi wake? Mungu anaona vita namna gani leo? Sehemu ya mwisho ya habari hii itajibia maulizo hayo.